Benta afya corner

Benta afya corner

Share

afya corner

Photos from Benta afya corner's post 10/09/2020

UGONJWA WA FANGASI ZA UKENI/ SEHEMU ZA SIRI
(VAGINAL THRUSH)

Ndugu zangu naomba nielezee kuhusu mwanamke na uke,kwa maana ya

UKE ni kiungo cha uzazi wa mwanamke, ambamo ndani yake kuna Lactobacillus bacteria na fangasi wazuri abao wako katika kiwango kinacho lingana/a balanced mix. Bacteria hawa na fangasi hizi husaidia sana kuulinda uke na maradhi mbalimbali endapo uwiano wake hauta bughuziwa. LActobacillus bakteria hutoa acid ambazo huzuia fangasi kukuwa au kuwa wengi zaidi.

UGONJWA WA FANGASI ZA UKENI ni ugonjwa anaoupata mwanamke endapo fangasi watakuwa wengi zaidi ya bacteria wazuri waliopo ukeni au k**a pH ya ukeni imezidi kiwango cha kawaida kinachopaswa(pH 3.5-4.5 ndio kiwango kizuri kiafya).

FANGASI ZA UKENI MARA NYINGI HUSABABISHWA NA FANGASI WAITWAO CANDIDA ALBICANS, LAKINI WAKATI MWINGINE NI AINA NYINGINE ZA FANGASI NA HIZI NI VIGUMU SANA KUTIBIKA

VITU VINAVYOWEZA KUSABABISHA UGONJWA WA FANGASI ZA UKENI

kunasababu nyingi sana baadhi ya hizo ni;

1.MATATIZO YA HOMONI(HOMONI ZA KUBADILIKA/KUWANYINGI SANA AU KUSHUKA SANA) hii inaweza kusahabishwa na; ukomo wa hedhi,ujauzito, (MP)kuwa katika siku za mwezi, matumizi ya dawa za kuongeza kiwango cha hormon za k**e

2. MATUMIZI YA ANTIBIOTICS hizi huuwa bacteria wazuri na kubadiri ph ya uke

3.KUFANYA MAPENZI NA MTU ALIYE NA UGONJWA WA FANGASI ZA SEHEMU ZA SIRI BILA KINGA

4.KUSHUKA KWA KINGA YA MWILI hii inaweza kusababishwa na magonjwa mbalimbali k**a UKIMWI, KISUKARI, UPUNGUFU WA MADINI,VITAMINI NA VIRUTUBISHI MBALIMBALI VYA MWILI.

5.ULAJI MBAYA HASA KUPENDELEA VYAKULA VYENYE SUKARI KWA WINGI (SUKARI NI CHAKULA KWA FANGAS HIVYO HUONGEZEKA).

6.KUKOSA USINGIZI NA MSONGO WA MAWAZO .

DALILI ZINAZOONESHA KUWA UNAUGONJWA WA FANGAS ZA UKENI

Kuna dalili nyingi sana k**a zifuatavyo;

~MUWASHO SEHEMU ZA SIRI

~VIPELE VIDOGO VIDOGO UKENI

~KUTOKWA UCHAFU MWEUPE AU WA RANGI YA KIJIVU UKENI WENYE HARUFU MBAYA

~VIDONDA AU MICHUBUKO UKENI

~KUYOKWA NA HARUFU MBAYA UKENI

~KUPATWA NA MAUMIVU MAKALI WAKATI WA TENDO LA NDOA

~KUVIMBA NA KUWA MWEKUNDU KATIKA MDOMO WA NJE WA UKE

~KUWAKA MOTO NDANI NA NJE YA UKE

KINGA YA FANGASI ZA K**E

1.EPUKA KUSAFISHA UKE KWA KUTUMIA VITU VYENYE KEMIKALI K**A SABUNI

2.EPUKA KUTUMIA MARASHI YENYE CHEMIKALI UKENI NA KUONGIZA VITU MBÀLIMBALI UKENI K**A VIDOLE, ASALI, MGAGANI N.K

3.EPUKA KUTAWADHA KUTOKEA NYUMA KWENDA MBELE BAADA YA KUJISAIDIA HAJA KUBWA AU NDOGO

4.MTIBU MPENZI WAKO ALIE NA UGONJWA WA FANGASI

5.SAFISHA UKE NA KUJIFUTA KWA KITAMBAA SAFI ILIKUUACHA MKAVU

6.HAKIKISHA KINGA YA MWILI WAKO IKO JUU

7.VAA CHUPI ZITENGENEZAVYO KWA VITU HARISI K**A PAMBA NA HARIRI

8.EPUKA ULAJI MBAYA WA CHAKULA HASA PUNGUZA VYAKULA VYENYE KUKUPAYIA SUKARI KWA WINGI MWILINI

9.TUMIA PADS ZISIZO NA KEMIKALI NA ZENYE VITU VYA KUKULINDA NA MAAMBUKIZI,KUKUFANYA UWE MKAVU NA HURU K**A BF SUMA SANITARY PADS

MATIBABU
UGONJWA HUU HUTIBIWA KWA VITU VIFUATAVYO

~VIDONGE VYA KUMEZA- ITAKUTIBU FANGAS, U.T.I SUGU, ILE AMBAYO BAKTERIA WAKE WA U.T.I WAPO KWENYE FIGO, PIA ITASAIDIA WANAWAKE WENYE MATATIZO YA KUTOPATA HEDHI AU MATATIZO YOYOTE YA HEDHI, MWANAMKE AMBAYE HASHIKI UJAUZITO, CANCER, KUONGEZA KINGA ZA MWILI, WANAWAKE WENYE MAUVIMBE(FIBROS) YAANI HII KIBOKO.

~MAJI YA KUOSHEA UKE,- ITAKUTIBU FANGAS, U.T.I KWENYE KIBOFU CHA MKOJO , YANASAIDIA KUWEKA UKE SALAMA,YANAONDOA UCHAFU WOTE ULIOPO KWENYE MIRIJA YA UZAZI, YANASAIDIA KUWEKA UKE KATIKA HALI YAKE YA MWANZO, INAONDOA FANGAS, NA MIWASHO SEHEMU ZA SIRI

~PEDI ZA BF SUMA=INASAIDIA FANGAS,INANYONYA KIMIMINIKA KINGI,NI NZURI KWA BAKTERIA WAZURI KUISHI,INANYONYA UCHAFU WOTE WA HEDHI,INAZIBUA MIRIJA YA UZAZI N.K.

N:B NI MUHIMU KUTUMIA DAWA ZA ASILI ZA VIRUTUBISHO NA KUACHA ZENYE KEMIKALI WAKATI WA KUTIBU FANGASI ZA UKENI.

KWA MAELEZO ZAIDI,
MAONI NA USHAURI
MATIBABU YA FANGASI SUGU NA ZA KAWAIDA KWA KUTUMIA DAWA ZA ASILI ZILIZO KATIKA MFUMO WA KISASA K**A VIDONGE,NA MAJI YA KUJISAFISHIA USISITE KUPIGA/TEXT/WHATSAP no.
07 19 42 44 71. au
07 62 56 26 62.

WOTE MNAKARIBISHWA....

08/09/2020

UJUE UGONJWA WA BAWASIRI NA ATHARI ZAKE

Bawasiri ni mojawapo ya matatizo ambayo mara nyingi inapotokea humfanya muathirika kuwa na aibu kuelezea au kwenda hospitali ili kupata tiba.Bawasiri husababishwa na kuvimba kwa mishipa ya damu aina ya vena katika eneo la mfereji wa haja kubwa.

A.KUNA AINA MBILI ZA BAWASIRI(HEMORRHOIDS)
1.Ya nje ya puru- Aina hii ya bawasiri hutokea katika eneo la mwisho kabisa la mfereji wa haja kubwa na mara nyingi huambatana na maumivu na muwasho katika sehemu hiyo.Mara nyingi mishipa hiyo ya damu(vena)hupasuka na damu huganda na kusababisha hali iitwayo THROMBOSED HEMORRHOIDS kitaalamu.
2.Ndani ya puru/tupu/duburi-Aina hii ya bawasiri hutokea ndani ya mfereji wa haja kubwa na haiambatani na maumivu hivyo kuwafanya wengi kutotambua kuwa wana tatizo hili.
Aina hii imegawanyika katika sehemu zifuatazo;
i.Bawasir kutotoka katika mahali pake(iliyosimama)
ii.Bawasir inayotoka wakati wa haja kubwa kurudi yenyewe baada ya kumaliza kujisaidia
iii.Bawasir inayotoka wakati wa haja kubwa na hairudi yenyewe baada ya kujisaidia mpaka mwathirika airudishe mwenyewe.
iv.Bawasir inayotoka wakati wa haja kubwa na ni vigumu mtu kuirudisha baada ya kumaliza kujisaidia.

B.NINI KINASABABISHA BAWASIR ?
Miongoni mwa visababishi vya bawasir ni;
-Tatizo sugu la kuharisha
-Kupata haja kubwa(kinyesi)kigumu
-Uzito kupita kiasi(OBERSITY)
-Ngono ya njia ya haja kubwa(ANAL S*X)
-Umri mkubwa na mambo yanayoongeza shinikizo katika tumbo.

C.DALILI ZA BAWASIR
-Kinyesi kuchanganyika na damu wakati wa kujisaidia CHEMATOZECHEZIA
-Maumivu au usumbufu katika njia ya haja kubwa
-Kutokwa na kinyesi bila kujitambua(kuvuja kinyesi)
-Kijiuvimbe katika eneo la tundu(mlango)wa kutolea haja kubwa.
-Ngozi katika eneo la tundu la haja kubwa kuwasha.
-Bawasir kutoka wakati wa kujisaidia haja kubwa.

D.ATHARI ZA BAWASIR
-Upungufu wa damu mwilini(ANEMIA)
-STRAGULATED HEMORRHOID
-Kinyesi kutoka na kuvuja bila kujitambua na kusababisha kunuka kinyesi saa zote.
-Kukupunguzia morali ya kufanya kazi kutokana na maumivu hasa watu wanaokaa muda mrefu maofisini.
-Kuathirika kisaikolojia
-Kukosa hamu ya tendo la ndoa.
-Kupungukiwa nguvu za kiume

E.JINSI YA KUZUIA BAWASIR
-Kula mboga za majani na matunda na nafaka zisizokobolewa kwa wingi
-Kunywa maji mengi lita sita hadi kumi na mbili kwa siku
-Punguza kukaa kwa muda mrefu chooni bila kutoa choo.

*Kwa maelezo zaidi na suluhisho wasiliana nasi kwa no. zifuatazo
07 19 42 44 71. au
07 62 56 26 62.

Photos from Benta afya corner's post 08/09/2020

TATIZO LA VIUNGO(JOINT PROBLEMS),

MIGUU KUWAKA MOTO, KUKAK**AA KWA MISULI, MAUMIVU YA KIUNO NA MGONGO, NICHANGAMOTO KWA WAZEE, WANAMICHEZO NA WANYANYUA VYUMA (GYM).

ya viungo,miguu kuwaka moto,maumivu ya kiuno na mgongo, yamekua yakiwasumbua watu wengi hasa wenye uzito mkubwa,wanaofanya mazoezi na wazee wenye umri kuanzia 55+
Hii ni kwasababu umri unavyozidi kwenda mwili unashindwa kuzalisha ute ute katika viungio vya mifupa,na hivyo kupelekea misuguano ya mifupa,ambapo husababisha maumivu makali sana na kupelekea mtu kushindwa Kukaa,Kuinuka,Kukimbia au Kutembea Kabisa!!

CHA TATIZO LA VIUNGO (JOINTS TEAR AND WEAR)

-Mara Nyingi Ugonjwa Huu Huitwa ARTHRITIS,Unasababishwa na hitilafu yoyote katika sehemu hizo za maungio ya mifupa.
Inaweza kuwa cartilage inalika,upungufu wa synovial fluid(Maji Maji Katika Maungio),maambukizi ya vijidudu katika moja ya maeneo hayo au mchanganyiko wa matatizo Mbali Mbali,Ikiwemo Uzito mkubwa.
Tabia kuu ya magonjwa haya ni maumivu kwenye maungio ya mifupa (joints) ambayo ni endelevu na ambayo hutokea eneo hilo hilo moja.

CHANZO CHA ARTHRITIS NI NINI?
Ili Upate Kuelewa Vyema Chanzo cha ugonjwa huu,hebu kwanza tutazame muundo wa joint au sehemu mifupa miwili inapokutana(Maungio).
Mfano Goti ambapo mifupa miwili mmoja wa paja na mwingine wa mguu vinapokutana:

Maungio ya mifupa-Ligaments;
-Ndicho kitu kinachoshikilia mifupa hii miwili pamoja,hii ni k**a utepe wa plastiki au mpira unaonyumbuka uliozunguka eneo hilo kwa nje,ukikunja goti inanyumbuka na ukinyoosha mguu inarudi.

Cartilage;Huu ni utando unafunika eneo ambalo mifupa hugusana ili kuzuia mifupa hii isisuguane moja kwa moja,Utando huu ambao kwa kiswahili tunauita gegedu huyawezesha maungio hayo kufanya kazi kiulaini pasipo kusababisha maumivu.

Capsule;Hiki ni kitu kinachofunika maungio haya kikizunguka pande zote,ndani ya mfuko huu wa capsule kuna synovial fluid ambayo huzalishwa na synovial membrane.
Synovial fluid ni ute ute wa kulainisha sehemu hiyo ya maungio na synovial membrane ni utando ulio kwenye kuta za ndani za capsule.

K**a nilivyoeleza hapo juu,kuwa kuna aina zaidi ya 100 za ugonjwa huu wa joints au arthritis.
Katika mada yetu ya leo tutatazama aina k**a nne hivi za ugonjwa huu,tukielezea chanzo cha kila aina....

#1. OSTEOARTHRITIS
- Hii ni aina ya arthritis inayosumbua watu wengi zaidi kuliko aina nyingine zote...
Ugonjwa huu huwapata zaidi watu wenye umri mkubwa,Osteoarthritis hutokea pale cartilage inapopoteza uwezo wake wa kubonyea na kuwa ngumu hivyo kuharibika haraka.
- Cartilage ni kiungo cha kuhimili migandamizo ya ghafla (shock absorber),Cartilage hii inapopoteza ubora wake,tendons na ligaments huvutika na kusababisha maumivu.
Hali ya uharibifu huu wa cartilage ikiendelea,mwishowe mifupa huanza kusuguana moja kwa moja na ndipo mgonjwa atakapoanza kupata maumivu makali sana sana.
- Athari za ugonjwa huanza taratibu na kuongezeka zaidi,Mgonjwa ataanza kupata maumivu kwenye joint baada ya kufanya shuguli fulani au baada ya mapumziko ya muda mrefu. Joints zitaanza kukaza siku hadi siku,Hasa wakati wa asubuhi unapotaka kuanza shughuli zako za kawaida.
Na siku zinavyosogea ndivyo utakavyoona ni vigumu zaidi kukitumia kiungo chako,Mara nyingine utaona uvimbe kwenye joint.
Osteoarthritis hushambulia zaidi nyonga,mikono,magoti na uti wa mgongo.

#2 RHEUMATOID ARTHRITIS.
- Ugonjwa huu hutokea pale mfumo wa kinga ya mwili unapopungua,viungo huanza kushambuliwa, ikiwa ni pamoja na synovial membrane (synovium) na kusababisha uvimbe na maumivu.
Hali hii isipodhibitiwa,huweza kusababisha ulemavu. Ugonjwa huu unaweza pia kushambulia macho,ngozi,mapafu,midomo,damu na mishipa ya damu. Huu ni ugonjwa ambao zaidi ni wa wanawake na huwatokea zaidi wawapo kati ya umri wa miaka 40 hadi 60.
Mgonjwa atasikia maumivu na kuona uvimbe kwenye joints za pande zote za mwili;
Yaani k**a ni magoti,yote mawili yatashambuliwa na Viungo vinavyoshambuliwa zaidi ni vidole,viwiko vya mikono na miguu.

- Athari zake huonekana zaidi asubuhi unapoamka na maumivu yanaweza kudumu kwa muda wa hadi nusu saa.
Muathirika wa ugonjwa huu hujisikia mchovu muda wote, hukosa hamu ya kula na hupungua uzito,Ugonjwa huu huweza kukua zaidi na Kusababisha matatizo katika viungo vyote vya mwili.
Matatizo yanayoweza kujitokeza ugonjwa ukikua ni k**a yafuatayo:
– Macho kuwa na ukavu,maumivu,wekundu,kutopenda mwanga na kutoona vizuri
– Midomo,Ukavu au kukauka kwa lips za midomo,maumivu na maambukizi ya fizi
– Ngozi,Vijinundu chini ya ngozi kwenye maeneo yenye mifupa
-- Mapafu,Kushindwa kupumua vizuri
– Mishipa Ya Damu,Uharibifu wa mishipa ya damu
– Damu,Upungufu wa chembechembe nyekundu za damu

#3. Infectious arthritis (septic arthritic).
- Aina hii ya arthritis inatokana na maambukizi ya bacteria kwenye synovial fluid. Maambukizi haya yanaweza kuwa pia ni ya fungus au virusi.
Wadudu kutoka sehemu nyingine ya mwili iliyo karibu na maungio ya mifupa huweza kusambaa kupitia mfumo wa damu hadi kwenye joint na kuleta maambukizi.

Mara nyingi mtu mwenye aina nyingine ya arthritis ndiye anayepata maambukizi ya namna hii,Mgonjwa ataanza kwanza kupata homa, maumivu na uvimbe kwenye joint.
Maeneo ambayo hushambuliwa zaidi na aina hii ya arthritis ni goti, mabega,kiwiko cha mkono,kiganja (wrist) na vidole na mara nyingi ni eneo moja tu ndilo litakaloshambuliwa

#4. Juvenile rheumatoid arthritis (JRA).
- Ni ugonjwa ambao huwapata zaidi vijana walio na umri ulio chini ya miaka 16 na unakuja kwa namna nyingi.
Kuna aina kuu tatu za ugonjwa huu:

I. Pauciarticular JRA.
- Huu ndiyo unaoonekana zaidi na hauna madhara makubwa ukilinganisha na aina nyingine,Mtoto atasikia maumivu kwenye joints zinazofikia nne.

II. Polyarticular JRA.
- Huu hushambulia joints nyingi zaidi, zaidi ya nne na maumivu yake ni makali zaidi.
Kadri siku zinavyoongezeka, ndivyo maumivu yatakavyozidi.

III. Systemic JRA.
- Huu huonekana kwa nadra ambapo maumivu hujitokeza kwenye maeneo mengi na madhara yake kuwa makubwa zaidi,Mtoto ataanza kusikia homa za vipindi ambapo huzidi zaidi nyakati za jioni.
Hali hii inaweza kumtokea mtoto kwa muda mfupi au kwa wengine kwa muda mrefu sana.
Mtoto atapata mauvimu kwenye maungio ya mifupa (joints),uvimbe kwenye maungio hayo na kukak**aa kwa viungo.
Mtoto huyu atakosa hamu ya kula hivyo kumfanya akonde.
Ugonjwa ukizidi, mtoto anaweza kudumaa (kushindwa kukua), ukuaji wa mifupa yake kuathirika na kupata matatizo ya macho (uveitis).

Changamoto Kubwa Ya Matatizo Ya Joints Huwapata Wana Michezo,Wanyanyua Vyuma(Body Builder),Watu Wanaofanya Kazi Ngumu,Mafundi Magari,Wabeba Mizigo Na Madereva Wa Masafa Marefu Na Wafanyakazi Wa Mahofisini Wanao Fanya Kazi Za Kukaa Zaidi.

SULUHISHO KWA MGONJWA MWENYE TATIZO LA JOINTS NA KUJIKINGA NA TATIZO LA JOINTS

Hakuna Ugonjwa usio na suluhisho k**a ukiuwahi mapema,japo pia ukichelewa ina kuwa ni mbaya zaidi ila suluhisho halikosekani kabisaa!!
Na Suluhisho pekee la Tatizo La Joints ni kutumia Virutubisho(Food Supplements),kwa mwenye tatizo ama kwa wanaofanya mazoezi ili kuongeza huo ute ute kwa lengo la kuzuia misuguano ya joints.

Kwa Ushauri au Maswali
Au Changamoto Nyingine Za Kiafya Tuwasiliane.....

0719 42 44 71 au
0762 56 26 62

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Arusha?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Website

Address

Kaloleni
Arusha