Latif BioCare Health Solution

Latif BioCare Health Solution

Share

NAWASAIDIA WANAWAKE KWA WANAUME KUTATUA MATATIZO YA KIAFYA KWA KUTUMIA PROGRAMU YENYE LISHE MAALUMU.

09/02/2023

FAHAMU KUHUSU MTINDO BORA WA MAISHA UNAOZINGATIA LISHE SAHIHI.
Muda gani tunakula na vyakula gani tunakula ni sehemu muhimu ya mtindo wa maisha ili kuwa na Afya njema.Kuzingatia aina ya vyakula kuna faida nyingi kiafya ikiwa ni pamoja na kuwa na uzito sahihi na kuepuka magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
Kutozingatia muda wa kula ni moja ya sababu zinazochangia mtu kutokuwa na Afya imara, Lakini pia uchaguzi usio sahihi wa vyakula husababisha ulaji wa vyakula usiozingatia mahitaji ya mwili.

:Kwa ELIMU ZAIDI na USHAURI WA KITABIBU unaweza kuwasiliana nasi,

https://wa.me/message/CRPX3LQSOZQ6M1

04/02/2023

FAHAMU KUHUSU VISABABISHI VYA TATIZO LA KICHEFUCHEFU (NAUSEA).
Kichefuchefu kwa kawaida huandamana na matatizo ya tumbo na hisia za kutaka kutapika.Huenda hali hii ikadumu kwa muda mfupi kisha kurejea mara kwa mara na ikadumu kwa muda mrefu.

Hali hii huchochewa na mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na;

↪️Ulaji wa baadhi ya vyakula.
↪️ Maambukizi katika mfumo wa utumbo.
↪️Vidonda tumboni.
↪️Aina tofauti za dawa.
↪️Kula chakula kingi kwa wakati mmoja.
↪️ Msongo wa akili.
↪️Kunywa pombe kupindukia.
↪️Mzio wa vyakula (Allergies).
↪️ Ujauzito.
↪️ Maumivu ya kichwa.
↪️ Utumbo kuziba.
↪️ Maumivu kutokana na ugonjwa wa kidole tumbo (Appendicitis).
↪️ Maradhi ya kibofu.
↪️ Maradhi ya kongosho.
↪️Homa ya uti wa mgongo (Meningitis).
↪️ Matatizo kwenye ubongo nakadhalika...

✍️Ni vyema sana kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu kwa kina ili kubaini chanzo halisi cha tatizo hili ili upate tiba inayokufaa zaidi.

:Kwa ELIMU ZAIDI na USHAURI WA KITABIBU usisite kuwasiliana nasi;
0766 972 073

Au bofya link hapo chini sasa hivi,

https://wa.me/message/CRPX3LQSOZQ6M1

01/02/2023

FAHAMU KUHUSU SABABU ZA MAGONJWA MBALIMBALI.

♻️MAGONJWA YA MAAMBUKIZI.
↪️Hewa.
↪️Kugusana.
Kushirikiana kimwili.
↪️ Kushirikiana kwa nguo.
↪️Kupewa damu na mtu yenye maambukizi (Blood Transfusion).

♻️ MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA.
↪️ Kuzaliwa na magonjwa (Genetic disorders).
↪️Uwepo wa KEMIKALI nyingi mwilini.
↪️Uwepo wa SUMU nyingi mwilini.
↪️ Matumizi ya vyakula vyenye madini ya ZEBAKI.
↪️Pombe (Alcohol Addiction)
↪️ Matumizi ya SIGARA (Ci******es Smoking).
↪️ Uzito wa kupindukia (Obesity).

✍️ Muhimu zaidi ni kuepuka na kuchukua tahadhari dhidi ya vihatarishi vya uwepo wa magonjwa mbalimbali.

:Kwa ELIMU ZAIDI, USHAURI WA KITABIBU na SULUHISHO LA MATATIZO MBALIMBALI YA KIAFYA wasiliana nasi sasa;
0766 972 073

Au bofya link hapo chini sasa hivi kuwasiliana moja kwa moja na mshauri,

https://wa.me/message/CRPX3LQSOZQ6M1

28/01/2023

TAKWIMU KWA MWAKA 2021/2022 ZA MAGONJWA AMBAYO HUWAKABILI WATANZANIA WENGI NA KUHATARISHA MAISHA YAO.
Zaidi ya 15% ya Wa-Tanzania hupoteza maisha kila mwaka kutokana na changamoto mbalimbali za kiafya hususani magonjwa yatokanayo na MFUMO WA MMENG'ENYO WA CHAKULA.

✍️Tafadhali usiwe miongoni mwao.Zingatia MTINDO BORA WA MAISHA kwa kutumia vyakula rafiki kiafya, pia fanya mazoezi mara kwa mara angalau dakika 30 kila siku.Muhimu zaidi hakikisha unatumia VIRUTUBISHO SAHIHI kuwezesha KINGA IMARA YA MWILI (IMMUNE SYSTEM) kujikinga dhidi ya maambukizi ya magonjwa mbalimbali.

:Kwa ELIMU ZAIDI na USHAURI WA KITABIBU wasiliana nasi sasa,
0766 972 073

Au Bofya link hapo chini sasa hivi,

https://wa.me/message/CRPX3LQSOZQ6M1

Photos from Latif BioCare Health Solution's post 26/01/2023

FAHAMU KINGA NA MATIBABU YA TATIZO LA KUKOSA CHOO
Matibabu ya tatizo la kukosa choo hutegemeana na ukubwa wa tatizo lakini mtu anaweza kupunguza na kuepuka uwezekano wa kupatwa na tatizo hili kwa kufuata kanuni za ulaji sahihi wa vyakula kwa sababu tatizo hili husababishwa pia namna unavyokula na kuishi, Hivyo ukifuata kanuni bora za ulaji wa vyakula tatizo hili halitakupata, Njia rahisi ya kuzuia kupatwa na tatizo hili ni kula NAFAKA ZISIZOKOBOLEWA, MATUNDA, MBOGAMBOGA na KUNYWA MAJI MENGI.
Matibabu huhusisha ukubwa wa tatizo ambapo kuna tiba mbili, Tiba ya kupewa DAWA, Lakini pia kufanyiwa UPASUAJI kuondoa kinyesi kilichoganda na kuendelea na matibabu ya kukufanya kuendelea kupata choo zaidi.

KUMBUKA: Zingatia kula milo mitatu, kula zaidi vyakula vyenye Nyuzinyuzi (High fibre diet), Kunywa maji mengi na fanya mazoezi mara kwa mara, pia usizoee kutumia dawa zenye kemikali mara kwa mara.

:Kwa USHAURI ZAIDI WA KITABIBU wasiliana nasi sasa;
TUPIGIE/TUTUMIE UJUMBE MFUPI KWA NJIA YA WHATSAPP;
0766 972 073

Au Bofya link hapo chini sasa hivi kuwasiliana moja kwa moja na mshauri,

https://wa.me/message/CRPX3LQSOZQ6M1

21/01/2023

FAHAMU KUHUSU TOFAUTI ZILIZOPO KATI YA VYAKULA VYENYE AFYA NA VYAKULA VYENYE KUDHURU AFYA ZETU.
Binadamu huhitaji chakula katika maisha yake yote.

Licha ya kuwa hutupatia NISHATI na VIRUTUBISHO mbalimbali lakini baadhi ya vyakula hivyo vinaweza kusababisha dosari na madhara makubwa kiafya.
...Wakati vingine hutuletea Afya na uponyaji.

✍️Na vyakula vyenye manufaa na vyakula vyenye madhara kiafya, Na hivyo vyakula vyote havina thamani sawa.Ukweli ni kwamba maamuzi tunayofanya kuhusu ulaji wa vyakula mara nyingi yanaathiri Afya zetu kwa kiwango kikubwa.Kadri tulivyo na TAARIFA na MAARIFA sahihi kuhusu vyakula vilivyopo ndivyo ilivyo rahisi kwetu kufanya maamuzi bora zaidi kuhusu Afya.

: Endapo basi ni Wewe, Ndugu au Rafiki yako amepatwa na mojawapo ya MAGONJWA kutokana na ATHARI za ulaji wa vyakula usisite kuwasiliana nasi kwa msaada zaidi;
SIMU/WHATSAPP;
+255(0) 766972073

Au Bofya link hapo chini sasa hivi kuwasiliana moja kwa moja na Mshauri;

https://wa.me/message/CRPX3LQSOZQ6M1

19/01/2023

Mfumo wa mmeng'enyo wa chakula (Digestive System) ndio Mfumo Mama wa Mifumo Yote Katika Mwili wa binadamu.Mfumo wa mmeng'enyo wa chakula ukiwa vizuri mwili utajenga kinga imara dhidi ya Magonjwa Mengi yasiyo ya lazima.

Hakikisha mfumo wako wa mmeng'enyo wa chakula unafanya kazi kwa kiwango chenye ubora siku zote.

:K**a ni wewe, Rafiki au ndugu yako anapitia katika mojawapo ya changamoto ya kiafya katika Mfumo wa mmeng'enyo wa chakula ni vyema basi uwasiliane nasi kwa msaada zaidi;

TUPIGIE/TUTUMIE UJUMBE MFUPI KWA NJIA YA WHATSAPP;
+255(0) 766972073

Au Bofya link hapo chini sasa hivi,

https://wa.me/message/CRPX3LQSOZQ6M1

Photos from Latif BioCare Health Solution's post 18/01/2023

Karibu sana katika ukurasa wetu maalumu kujielimisha bure Njia Rahisi Za Kuondokana Na Matatizo Ya Kiafya Bila Kutumia Madawa Makali Ya Hospitali.

Photos from Latif BioCare Health Solution's post 18/01/2023

Kwa Majina naitwa Abdulatif Abubakar .Ni Mtaalamu wa Afya kwa Magonjwa ya Mmeng'enyo Wa Chakula kwa kutumia Programu iliyosheheni LISHE MAALUMU.
Kwa miaka mitatu sasa nimekuwa nikiwasaidia WANAWAKE kwa WANAUME kuwaelimisha namna ya kutatua changamoto zao kwa mfumo wa LISHE MAALUMU.

Want your business to be the top-listed Beauty Salon in Arusha?
Click here to claim your Sponsored Listing.

Category

Telephone

Address


Arusha

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Saturday 09:00 - 17:00