Bright Future Care4731
Nawasaidia wanawake wenye kusumbuliwa na changamoto ya uzaz kwa vyakula asilia
26/03/2024
Ugonjwa Wa Pid:
Ugonjwa wa pid ni maambukizi katika viungo vya uzazi vya mwanamke. Maambukizi haya kutokea ikiwa bakteria wanaoambukiza kwa njia ya kujamiiana watasambaa kutoka kwenye uke kwenda kwenye mji wa mimba (uterus), mirija ya uzazi (fallopian tubes) na kwenye O***y (ambapo mayai ya mwanamke hupatikana).
Picha Za Ugonjwa Wa Pid:
Leo katika makala yetu tutazungumzia sababu zinazoweza kupelekea mwanamke kupata ugonjwa wa pid na tiba yake.
Sababu Za Ugonjwa Wa Pid:
Zifuatazo ni sababu zinazochangia mwanamke kupata ugonjwa wa pid ambazo ni pamoja na;
1) Magonjwa Ya Zinaa.
Magonjwa ya zinaa k**a vile kisonono (gonorrhea) na pangusa (chlamydia) yanaweza kuchangia mwanamke kupata ugonjwa huu wa pid. Mwili wa mwanamke unapokuwa na afya njema, mlango wa kizazi (cervix) huwa na uwezo mkubwa wa kuzuia bakteria wasiweze kuingia katika viungo vya ndani vya uzazi kutoka ukeni.
Hata hivyo wakati mlango wa kizazi unapokuwa wazi na kuruhusu magonjwa ya zinaa kuingia hasa kisonono (gonorrhea) na pangusa (chlamydia), mlango wa kizazi hupata maambukizi na kisha hupoteza uwezo wake na hivyo kuruhusu maambukizi na bakteria kuingia na kufika juu kwenye viungo vya uzazi.
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Website
Address
Arusha Mianzini
Arusha
